Wanasema visa vya ufisadi na mapendeleo vimeongezeka sana.
Makundi yaliyoandaa maandamano hayo yamekuwa yakitumia
kitambulisha mada #zumamustfall kutafuta uungwaji mkono mtandaoni.
Maandamano hayo yamefanyika Siku ya Maridhiano, siku ya
mapumziko ambayo lengo lake ni kuleta pamoja watu wa asili mbalimbali Afrika
Kusini.
Jana Bw
Zuma, akiongoza sherehe za kuadhimisha Siku ya Maridhiano, ameahidi kukabiliana
na ukosefu wa usawa miongoni mwa watu wa asili mbalimbali.
Hakuzungumzia maandamano dhidi yake.
0 comments:
Post a Comment