Thursday, 17 December 2015

on Leave a Comment

Uuzwaji wa Matunda yaliyo Katwakatwa Wapigwa Marufuku


Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Ummy Mwalimu amepiga marufuku biashara ya uuzaji wa  matunda yaliyokatwakatwa pamoja  na uuzaji wa chakula katika mazingira yasiyo salama ili kukabiliana na ugonjwa wa KIPINDUPINDU ambao umesambaa katika mikoa 21 ya Tanzania Bara

Akitoa taarifa ya hali ya ugonjwa wa KIPINDUPINDU nchini Waziri  Ummy Mwalimu  amewasisitiza maafisa afya kuwasimamia wajasiriamali  wanaofanya biashara ya chakula na kuhakikisha wanazingatia kanuni za afya.



0 comments:

Post a Comment