Samatta anawania hiyo na wachezaji wengine
wawili Baghdad Boundjah wa Algeria na Etoile du Sahel na Kipa machachari wa TP
Mazembe ya DR Congo Robert Kidiaba.
Nyota huyo ameingia kwenye kinyang”anyiro
hicho baada ya kuwa mfungaji bora wa klabu bingwa barani Africa nae baghdad
akiwa kama mfungaji bora wa michuano ya kombe la shirikisho na Kidiaba
akiiwezesha Mazembe kutwaa ubingwa wa africa.
Kwa upande mwingine Siku chache tu baada ya kutawazwa kuwa mchezaji bora wa Afrika na shirika la BBC Yaya Toure, ametajwa miongoni mwa wachezaji watatu bora kuwania tuzo ya mwanakandanda bora mwaka huu na Shirikisho la soka barani Afrika .
Nyota huyo wa Manchester City kwa mara
nyengine atakuwa akipigania tuzo hiyo dhidi ya mshambulizi wa Black Stars ya
Ghana na Swansea Andre 'Dede' Ayew na Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon na
Borussia Dortmund.
Mshindi atachaguliwa na makocha wa timu za taifa na kutangazwa katika dhifa maalum Januari tarehe 7 mwakani.
0 comments:
Post a Comment