Serikali ya awamu ya tano imeanza kutimiza kwa vitendo kauli ya
kuifanya sanaa kuwa moja ya shughuli za kiuchumi baada ya kupitisha sheria
ambayo inavitaka vyombo vya habari hapa nchini kuwalipa wanamuziki pindi
wanapotumia nyimbo zao.
Waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji CHARLES MWIJAGE amesema
sheria hiyo itaanza kufanya kazi JANUARY MOJA mwaka 2016 huku waziri wa habari,
utamaduni , sanaa na michezo NAPE NNAUYE akisema sasa wameanza kutekeleza yale
waliyoyapanga kuyanfanya kwenye kukuza sanaa hapa nchini.
Katika kutimiza suala hilo chama cha hakimiliki hapa nchini
(COSOTA) kimeingia mkataba na kampuni ya CMEA ili kuweza kufuatilia mapato ya
kituo cha RADIO au TELEVISION inayopiga kazi ya mwanamuziki na kuweza kujua
malipo yake yawe ya namna gani kwa mwezi.
0 comments:
Post a Comment